Saturday, 7 January 2017

*MAJIRA NA NYAKATI ZA KUISHI JUU YA UMBO


Wakili wa MUNGU leo ameanza ibada kwa kutangaza kuanza Rasmi kusimamishwa kwa chujio la Haki namba tatu.

Amesema kusimamisha majira na nyakati za Umoja wa MUNGU, Kristo na Kanisa imetufikisha kuwa juu ya umbo. Kizazi cha 1 hadi 4 wote waliishi kwenye mwili. Kizazi cha nne Eliya Ad2 alituingiza kwenye viungo.

Hatahivyo Wakili wa MUNGU aliongoza wenye haki kutoa sadaka maalumu ya kuondoa vya Mti, udongo na vile ambavyo havina heshima.

Nakusema kuwa kila ambacho sio cha heshima kwako leo ni mwisho kwa sadaka maalumu ya leo.

Sadaka hii inasimamisha vya fedha, dhahabu na mawe ya thamani vyenye heshima na utukufu 2Tim2:20-21 na 1kor 3:10-12. Vyombo vya miti, udongo vimefutwa maana havina heshima.

Kila aina ya mila na desturi tabia ya lugha ukoo kabila vilivyokuwa vinazuia wewe kutoka leo vinaungua kwa sadaka hii, hata kama umbo la mila na desturi lilizuia kichwa wako kuokoka leo yanaungulia hapa.

Mwenye nyumba halisi ametinga ndani ya nyumba yake Mt 21:41, mafarakano kwenye agano lako leo mwisho, yote uliyowahi kuona wameshindikana leo ni mwisho, yote uliyowahi kujiuliza sana ndani yako leo unapokea majibu.

Malaika wa kusachi kuondoa maumbo yote kinyume na MUNGU. Kila aliyekanyaga hapa na kila anayesikia sauti hii imtoe kila mahali alipokuwa amekwamia.

Akifafanua kuwa kila jambo lisilofaa linateketezwa hapa kwa sadaka tunayompa MUNGU.

Sheria iliyokuwa imeng'anga'ania leo tumetoka tupo juu ya umbo, ubishi ndani ya Agano la kichwa na kanisa binti na kijana leo tumeshinda.

Ikiwa ni pamoja na kutawaliwa na mabwana wengine leo mwisho, umbo la ukoo, kabila, mila na desturi leo zimefutwa milele kwa Damu ya MUNGU. Sio saa ya mishale bali ni saa ya shangwe nderemo nk.

Kizazi cha 1-3 kwasababu

🌺Kizazi cha 1 kilikuwa manung'uniko na malalamiko.

🌺Kizazi cha 2 kilikuwa na sheria ya dhambi.

🌺Kizazi cha 3 kilikuwa NENO lililovaa mwili kanisa nalo lilikuwa mwilini.

🌺Kizai cha 4 tulitolewa mwilini na kupelekwa kwenye viungo.

🌺Kizazi cha 1-4 wote tulikuwa tunakutania kwenye umbo.

*Aidha Wakili wa MUNGU amefunua mambo 12 ambayo ni halisi ndani ya wenye haki baada ya kufuta kabisa mwili, viungo na umbo*

1.) Ufunuo 22:4 tutakuwa tukimwona MUNGU uso kwa uso.
2.) Ufunuo 21:3 Yohana katka miaka 2000 iliyopita akiwa patmo aliona maskani ya MUNGU ikiwa katikati ya "watu"

3.) Ufunuo 1:8 mimi ni mwanazo na mwisho niliyekuwepo niliyepo nitakayekuja sasa amekuja na kila jicho litamuona. Na sasa amekuja kuishi na wenye haki.

Kwenye dini hatujawahi kuambiwa kuwa MUNGU amesema atakuja ila walituambia Yesu atakuja. Amekuja ili wote tufanye kazi nae, mwendeshe gari nae, muimbe wote, mcheze wote nk.

4.) Ufunuo 20:6 watakao mwamini watakuwa Makuhani wa MUNGU na Kristo wake. Amesema kinacholeta shida mikoani sasa ni kwasababu walishazoea kuamka na kwenda kuongea wanachotaka wao kumbe wasijue MUNGU alishakua.

5.) 1kor15:25-28 ni sharti amiliki yeye. Atakuwa ni Kichwa cha Kanisa.

6.) Mathayo 21:41 alisema akija ataangamiza vibaya wabaya wote imekwishatokea ila ni kwa wale tu waliokubali kuishi juu ya umbo.

7.) 1Petro3: 13-14 akija mbingu zitaungua yaani mifumo yote itaungua viumbe vya asili vitatketea. Mtapata mbingu mpya na nchi mpya ambayo haki yakaa ndani yake.

8.) Isaya 65:20-25 simba kula nyasi. Ukijenga nyuba utakaa, ukilima shamba utakula wewe, hutazaa kwa taabu, hatutapata taabu maana amekuja mwenyewe aliye chanzo cha Baraka.

9.) Mathayo 16:16-19 hasa "18" sasa Kanisa linatawala malangfo ya kuzimu kwa uhalisi. Maana ni majira ya MUNGU kulijenga Kanisa ambalo malango ya kuzimu hailishindi.

10.) Yohana 4: 23-24 Yesu alisema saa ipo ambayo waabuduo watamuabudu MUNGU katika roho na kweli. Na kituo cha uhalisi tumeshafika yaani yote ambayo MUNGU aliahidi sasa ni muda wa kuyapata.

11.) Ebr 8:10-12 wote watamjua MUNGU aliye mdogo na aliye mkubwa hivyo dhambi na uovu kufutwa milele.
NB:-
*TUMEFIKA MAHALI PA UWEPO WA VITU PALE MLIMA WA MOTO HAVITAPUNGUA*

12.) Yeremia 50:20 na Ebr 8:12 uovu kufutwa ndani ya Kanisa. Utatafuta dhambi hutaiona. Tumehama kabisa kituo cha umbo tunaishi juu ya umbo.

Hatahivyo Wakili wa MUNGU alisema ndani ya Kanisa bado kuna umbo la Edeni Mwa 2&3 Ambapo alisema bado kuna mwingiliano wa safu kati ya kichwa, kanisa na watoto katika familia.

Aidha Wakili amesisiiza kila familia kutenga kiti maalumu cha kukaa baba wa familia tu na kiti maalumu cha kukaa mama wa familia tu ambapo viti hivyo visikaliwe tena na yeyote mwingine kwenye familia.

Lakini pia ameshukuru kwaajili ya kila waliotii NENO la kushiriki karamu kwa umoja na kusisitiza kuendelea kila familia kushiriki karamu kwa mkono pamoja ikiwa ni Agano la umoja kwa familia nzima.

Mwa 18: amesema umoja huo ndio ambao unaitwa KUSHIRIKI pamoja na MUNGU, Kristo na Kanisa na kuongeza kuwa "nataka mataifa yote wajue kuwa kuna kizazi cha MUNGU na ijulikane kuwa tabia ya MUNGUna Kristo ndani ya Kanisa imesimama"

    

   

Thursday, 5 January 2017


      KUISHI JUU YA UMBO


WAKILI wa MUNGU leo ameanza ibada kwa kujibu maswali mawili ambayo jana aliulizwa na Wakamilifu kwa lengo la wote tupate ufahamu kwa pamoja.

Swali aliloulizwa ni “kanisa tunafuta umbo la nyoka lakini umbo la nyoka hatujawahi kuliona kanisani?”

Akajibu kwa kusema “nyoka ana ndimi mbili, maana yake ni:-
  1.) ulimi mmoja ni wa mema.
  2.) ulimi wa pili ni wa hila.

Alisema tunaposema umbo la nyoka maana yake ni hila. Kanisani kulikuwa na wenye ndimi mbili. Hivyo MUNGU amefuta wale wenye ndimi mbili kanisani.

Hao wenye hila walikuwa wanachaua wenye haki wasimfahamu Wakili ni nani kwasababu wanajua usipo mfahamu huwezi kupokea kutoka kwa MUNGU.

Waovu walikuwa wakiwavulia wenye haki uchafu wao na kusababisha wenye haki kukosa haki zao ingawa wanaomba kwa bidii. Sasa MUNGU ameweka mwisho wa hizo ndimi mbili.

Swali la pili:-
Nitajuaje kama nina umbo la nyoka ? alijibu kuwa kulikuwepo na waliouza nafsi zao kwa kujua na wengine waliibiwa bila kujua.

Wapo waliouza nafsi zao kwa kerubi wakaja kanisani wakiwa na moyo na roho hawana nafsi ili waishi lazima waibe nafsi ya wenye haki kwa kuwavulia matakataka yao hivyo ndivyo MUNGU amefuta kuibiwa.

Hatahivyo aliongoza wenye haki kutoa sadaka Maalumu ya wote kuja kujisalimisha kwa MUNGU Madhabahuni kwakuwa MUNGU ni halisi, waabuduo halisi na kanisa ni halisi.

Sadaka hiyo inarejesha wote waliondoka kwa kudanganywa ikiwa ni pamoja na kuwaleta ndugu zetu tunaotaka waje kwa MUNGU Aliyetuma wote.

Aidha Wakili wa MUNGU ametaja aina za chujio la Haki ambalo kanisa tumepitishwa na MUNGU mwenyewe hadi kufika mahali pa kizazi cha MUNGU kimefika:-

1.)Chujio la kutenga kondoo na mbuzi. Mbuzi na kondoo hao kuchujwa kupitia malaika wa MUNGU, kristo na wa Wakili wa MUNGU.

2.) Chujio la Toba ya MUNGU. Ambayo imeondoa magugu.

3.) Chujio la umoja wa Baba, Kristo na Kanisa kutusafisha kwa upya ili kuondoa umbo la nyoka.

Mt 12:32 makuhani wa MUNGU kizazi cha MUNGU ni Roho atakae mgusa anashuhulikiwa na MUNGU mwenyewe.

UMBO
Wakili wa MUNGU amesema tunapozungumzia umbo maana yake ni zile tabia tulizokuwa nazo kutoka kwenye kabila, koo, lugha, taifa nk.

Lakini MUNGU anataka wenye haki tutoke mahali pa umbo laaina yoyote na tuende kuishi juu ya umbo maana umbo linasababisha tusimwelewe MUNGU.

Mwanzoni kanisa tulikuwa tunajipatanisha au kuungana na Nabii yaani hapo Nabii alikuja kwakuwa alitumwa lakini Sasa hatuungani tena bali tunamwalika Wakili wa MUNGU ili kuja na jeshi lote la MUNGU hapo ulipo.

Amesema tumekuwa tukishindwa kuwaleta wengine kanisani kwasababu tumekuwa na umbo kama wao wakati tunatakiwa kuishi juu ya umbo.

Faida ya kuishi juu ya umbo ni pamoja na:-
#kutetewa na MUNGU na uumbaji wote.
# Mhub3:14 Najua maana yake Hakika (ufahamu)kila anachofanya Wakili ni MUNGU anafanya.
#Kila kazi aifanyayo MUNGU itadumu milele. Kuzifuta kazi hizo haiwezekani.
#Hauwezi kuiongeza kitu chochote.
#Hauwezi kupunguza kitu.
#MUNGU amefanya hivyo ili wamche yeye.

Mhubiri 3:17-22 Wakili wa MUNGU alichukia kuishi kwenye viungo na umbo kwa kuwa hakutaka  kufanana na mnyama.

Aidha amemtaka kila mwenye haki kukubali kuhama kuishi kwenye umbo kwani kuishi kwenye umbo ni maisha ya kufanana na mnyama hivyo uishi juu ya umbo.


KUSIMAMISHA SIKU 7 ZA ADENI NA EDENI ISIYO NA UMBO LA NYOKA


Wakili wa MUNGU amesema kila siku ina msingi wake na jengo lake ambapo kazi ya msingi ni kuchora ramani.

Aidha alizungumzia Eb1:14 na Eb 1:5 kuhusu utendaji wa ibadi kubwa ya malaika ambao MUNGU amewaachilia malaika wengi wasio na idadi kwaajili kumuhudumia kila mmoja.

Yaani kwajili ya somo, kukuongoza, uponyaji, kuelewa, fedha, Baraka na kila kitu kulingana na mahitaji yako 1 Petro2:9-10 sisi tuna ukuhani wa kifalme ambao tunahudumiwa kwa kila kitu.

Kuna malaika wanaonihudumia na kuhakikisha ninapata kila ninachokihitaji isaya 44:26 kwamba MUNGU anathibitisha NENO litokalo madhabahuni Isaya 45:7-8 MUNGU anathibitisha NENO ninalotamka hivyo nitamke ili kuumba siku yangu kwani nina nguvu hiyo.

1yoh4:17 kama MUNGU alivyo ndinyo tulivyo hivyo tamka vitu vizuri na halkikisha unaweka ulinzi kwa kila unachotamka kwa akukiumba kila siku.

Hatahivyo Wakili wa MUNGU ameongoza wenye haki kutoa sadaka maalumu ya kusimamisha siku 7 za kufuta umbo la nyoka ndani yetu.

Uumbaji wote tunaouona upo katika Adeni na Edeni. Mlima wa BWANA inamaanisha BABA, NENO na Roho.

Adeni ina maana ya mkusanyiko wa NENO la MUNGU na Edeni ni Bustani ya BWANA.

Adeni ni marejesho ya vituo vyote vya Rohoni (mkusanyiko wa Ufahamu wa NENO ambao haujaibiwa.)

Edeni ni Bustani ya Kanisa. Edeni ni nafsi inayomjua MUNGU. Maisha yote yanapatikana ktk Adeni na Edeni.

Kanisa lilitakiwa kukaa katka Adeni na Edeni lakini walitolewa zikaa dini na madhehebu na dunia.
Biashara yako na kazi yako ikiwa ni pamoja na kila kinachotajwa kwa majina yako kinatakiwa kukaa Adeni na Edeni.

Kukaa Adeni ni kukaa na BABA na NENO na mimi nikiwa ni Roho. Kukaa Edeni ni mimi au nafsi yangu kumjua MUNGU.

MTIRIRIKO WA UUMBAJI WA MUNGU
Ufu 12:1 mwanamke
Ufu 12:3 nyoka
Ezekel 28:15 Adeni.
Mwa 1:1 mbingu na nchi
Mwa 1:3-31
Mwa 2:1-4
Mwa 2:15 Edeni
Mwa 3:1 nyoka

Kutoka MUNGU kilichofuata ni nyoka. Kabla hujakutana na MUNGU nyoka na kabla ya kumjua MUNGu ulimjua kerubi na nyoka kwanza.

Kaba ya kukutana na Wakili wa MUNGU anaezuia ni nyoka. Nyoka anakusababisha nafsi yako isimjue MUNGU kwa maana ya kukaa Edeni.

"kabla sijaja mimi hapa mnatakiwa mpige kwanza nyoka anayevuruga ufahamu usielewe wala kukumbuka na MUNGU hawezi kukupa kile usichokifahamu wala kukikumbuka" alisema Wakili wa MUNGU.

"MUNGU amekuja kuishi na sisi akiwa ni BABA hivyo usikubali shida yoyote ikufanye usiwe na furaha wala kukosa amani maana MUNGU anasovu yote hayo" amesema Wakili wa MUNGU.

"Jambo lolote usipolipiga halitoki na ulipige katika majira yake, sasa majira ya kupiga umbo la nyoka imefika piga umbo hilo ili MUNGU atamalaki katika maisha yako" aliongeza Wakili wa MUNGU.

Kulikuwa taasisi Fulani zimeweka nembo ya nyoka kwa kuwa wajua ya kuwa nyoka ni mwelevu. Ndio umbo la nyoka lilikuwa linaendelea kufanya kazi.

Tuesday, 3 January 2017


MADHABAHU YA UMOJA WA MUNGU, KRISTO NA KANISA


Wakili wa MUNGU leo amesema tumefika mahali pa kuachana na umbo la vizazi vilivyopita Mdo2:34- kwani lile umbo la mwili lilisababisha Kristo kwenda mbinguni na maadui ndio maana aliambiwa kaa pembeni kwanza mpaka maadui zake awaweke chini ya miguu.

Utawala wa amani umesimama na MUNGU amekuja ndipo adui anakimbia uso wa MUNGu kwa mimi kutolipa kisasi kwa kuwa kisasi ni cha MUNGU.

Aidha Wakili wa MUNGU ameongoza wenye haki kutoa Sadaka maalumu ya kujenga madhabahu ya umoja wa MUNGU, Kristo na Kanisa 1wafalme 13:4-6.

Kwa sadaka hii itadhihirisha wazi wale wenye wepesi wa kuonea wengine na kupiga wengine na kusema "yeyote anayetaka kukupiga kofi mkono utakatika, atakaye kunyoshea kidole mkono utabaki hivyo hivyo na atakayeomba maombi mabaya na kumsengenya mwingine mdomo utaenda upande na atakuwa bubu".

Aidha kabla ya kutoa sadaka maalumu hiyo alilivua Kanisa mwonekano wote wa zamani kwa Toba ilithibitisha MUNGU yupo juu ya nchi yaani anayekugusa akutane na MUNGU kwa kushughulikiwa saa hiyohiyo. Lazima kuhakikisha mwenye haki analindwa na jambo hili lazima litokee.

Amesema dunia ilichukua nafasi ya MUNGU kwa kuchukua namba moja ili kanisa lisifike majira ya saba tuishie majira ya sita kwa mahesabu ya saba kutoa moja kanisa likabaki na majira ya sita hadi hapo MUNGU alipolifunulia kanisa kuhusu majira ya saba na sasa tumeingia kwa uhalisi maana namba moja imepatikana.

Hatahivyo alifanya ufafanuzi wa vizazi vyote na utawala wake kuwa kizazi cha kwanza hadi cha nne kilitawaliwa na mwili,viungo na umbo.

Alisema viungo ni vya ndani, kwa nje ni mwili na umbo linaonesha tabia yako ambapo kulikuwa na ushirikiano kati ya mwili, viungo na umbo ambao sasa tunaushirikiano wa MUNGU, Kristo na Kanisa lakini ni baada ya kufuta ushirikiano wa mwili, viungo na umbo.

Amemshukuru MUNGU kwa kizazi hiki kuwa juu ya mwili, viungo na umbo ambapo sasa Kanisa kwa ushirikiano wa MUNGU, Kristo na kanisa halina mwili, viungo wala umbo ambapo sasa MUNGU yupo kila mahali mwenye haki alipo na anafanana hivyo hivyo ilimradi mwenye haki huyo anatenda kwa haki.

Aliyataja Mambo ya kushughulikia ili kufuta kabisa mwili, viungo na umbo kwa kila mwenye haki kuwa ni pamoja na:-
Moyo- kwa kuungana na moyo wa MUNGu

Kiuno- kufunua mambo mazuri.

Tumbo-lizae vitu vizuri.

Macho-yaone mazuri tu.

Kifua- tupokee haki ya MUNGU.

Damu- kuugua, magonjwa hayapo tena.

Pumzi- utamke Baraka.

Mabega- yawe ya haki, furaha na amani.

Masikio- kusikia NENO na lizae matunda.

Kitovu- kurithi kutoka kwa MUNGU.

Uti wa mgongo-tumaini lako liwe MUNGU tu

Ulimi- unene NENO tu.

Sauti- yako iungane na sauti ya saba.

Mikono-kazi zote ziwe kwa utukufu wa MUNGU.

Koromero- utoe sauti ya MUNGU tu.

Aidha Wakili wa MUNGU alihitimisha ibada hiyo kwa kufafanua umbo la kufuta katika agano la kichwa na kanisa lililokuwa likimzuia MUNGU asitamalaki katika familia ambalo akaliita Umbo la bustani ya edeni.

Alisema hilo ni la kila mmoja ndani kanisa analotakiwa kulifuta kuwa ni kwamba Adamu ingawa alipewa maelekezo yote na MUNGU kuhusu kila kitu cha kulima na kutunza bustani ya edeni lakini yeye hakutoa taarifa na maelezo yote kwa mkewe Hawa na kusababisha kukalia kiti cha aliyepewa maelekezo yote ambae ni Adamu.

Hata hivyo Wakili alisisitiza kila mmoja kutanguliza toba ya kina kuanzia bustani ya edeni kwaajili ya kichwa kutokutoa taarifa kamili kwa kanisa wake, kanisa kukalia kiti cha kichwa na kichwa kikalia kiti cha kanisa kwa lengo la kurejesha Mlima wa Bwana na mahali pa Bustani ya Edeni kwa uhalisi Ezek 28:15 na Mwa 2:15.

Na ndipo alijenga Madhabahu hiyo ya Umoja wa MUNGU, Kristo na Kanisa ambayo itasimamishwa kwa siku saba. 


KUFUNULIWA KWA KANISA AMBALO NI UMOJA NA MUNGU NA KRISTO MILELE


Kiti cha MUNGU, Meza ya MUNGU na fimbo ya MUNGU vimerejea ndani ya kanisa (Mlimani kwa MUNGU).

Akijenga msingi wa Ibada hiyo Wakili wa MUNGU ameongoza wenye haki kutoa sadaka maalumu inayonipa kuketi pamoja na MUNGU nikiwa namilikiwa na (Baba, Neno, Roho na Kanisa) iliyounganishwa na hakika ya NENO na Heshima ya NENO.

Neno lililozuia nisipotee lipo ktk 2 wafalme 5:20-26.

MUNGU anatuona lakini tumekuwa tukimdanganya Wakili wa MUNGU nakakwamba hatuoni kila tunapokuwa.

 Amesema dunia imetengeneza makuhani wamdanganye Wakili wa MUNGU ili alie lakini Wakili wa MUNGU halii.

MUNGU nakushukuru kwa kuwa umoja wako umeonekana ndani yangu kila mahali nitakapokuwepo.

Umbo la kizazi cha kwanza ni manung'uniko, malalamiko, vilio na kumchukiza kiongozi.

Umbo la kizazi cha pili ni kufundishwa kweli na kuikataa na kuvunja madhabahu ya MUNGU.

Umbo la kizazi cha tatu lilikuwa ni kuendelea kukataa yale yanayofunuliwa kama ilivyokuwa katka Yoh 6:30- hasa kilichosababisha kutopokea ufunuo ni tabia ya mwili.

Umbo la kizazi cha nne lilikuwa la tabia za vizazi vyote kuanzia kizazi cha kwanza hadi cha tatu.

Rumi8:4-7 nia ya mwili ni mauti hata vile tulivyoingia zaidi ya viungo kwa kuwa tulikuwa na nia ya mwili ilikuwa ni lazima mauti ingetupata, lakini MUNGU anataka tuwe na Roho ya Uzima kwa kuwa nia zetu ni za Roho ambayo ni uzima.

Kuongea na kuhoji hoji sio tabia ya MUNGU. MUNGU atanionyesha mambo mengi iwapo nitakuwa na tabia ya kunyamaza kimya na kusubiri majira hivyo niache tabia ya kuona jambo na kuongea nilichoona.

Kila mwenye tabia ya kushindana na mwingine ni kwakuwa anatabia ya au kile kilichompata Hawa.

Mambo ya kufuta yanayofatana na mwenye umbo la mwili:-
Mwa 3:1-6 hiki ndicho kilichompata Hawa kutaka kukalia kiti cha MUNGU.

Mwa 5:3 tabia ya mtu ya kupanda na kushuka.

Tabia ya kujitetea ni tabia ya Adamu na ni tabia isiyofaa mbele za MUNGU kwani imesababisha wengi kujitetea na kuwa sukumia makosa wenegine.

Kujitetea ni tabia ya mwili au umbo la mwili na viungo hivyo nilazima nitoke kwenye viungo na umbo la mwili.

Tunaweza kuishi kama Wakili wa MUNGU kuto kuwa na principle za maisha ya mwili na viungo na umbo lake. Sitakiwi kuadilika badilika tabia.

Habari ya Musa Kut 32:1-6 na Hesabu 2:9-10 Musa alikuwa mwepesi wa kutubu kwaajili ya wengine lakini kwaajili yake alikuwa hawezi.

Hiki ndicho kinachompata Yule anae tubu kwaajili ya wengine lakini yeye mwenyewe hatubu inasababisha kuchoka kutenda mema.

Tubu kwa kile ulichofanya na usichofanya huo ndio utakatifu MUNGU anaoutaka. Tuwe na tabia ya toba binafsi.

Tabia ya kusanyiko la MUNGU la kizazi cha kwanza lilikuwa na manung'uniko.

"MUNGU tusamehe kwa ajili ya Kanisa la jangwani kwa kuwavusha lakini kwa muda mfupi walinung'unika.

Sisi leo kukatae tabia ya tumbo ya kutokusema asante Mt17:1-8.


UMOJA WA BABA, NENO NA KANISA

MUNGU ni Alfa na Omega ni mwanzo na mwisho, aliyepo atakayekuwepo ataendelea kuwepo Uf 1:8.

MUNGU aliruhusu NENO livae mwili. Luka 2:21 mtoto Yesu alipozaliwa aliitwa  Yesu ni NENO lililovaa mwili baadae NENO lilipakwa Mafuta ukaitwa Yesu Kristo NENO lina Moyo, Roho na Nafsi.

MUNGU kabla hajaumba chochote alikuwa na ufahamu wa NENO na alikuwa anafanya kazi peke yake. Tunda la roho ni heri tisa Mt 8:30 na Yoh1:1-5.

BABA=MUNGU –Roho, moyo, Nafsi
NENO - Moyo, Nafsi na Roho.
ROHO – ina Moyo, Nafsi, Roho.

Kitu ha kufurahisha leo ni kwamba “sisi leo tumepata Neema ya kuingia kwenye shamba”

Sasa Kanisa tumeingia ktk kituo cha uhalisi
*Kanisa
*Kristo
*MUNGU.

Hatahivyo Wakili wa MUNGU ameongoza wenye haki kutoa sadaka maalumu ya kurejesha nguvu ya kutoa ikiwa ni pamoja na kutoa kupitia masirika mbalimbali ya misaada ya kimataifa.

Amefafanua kuwa dunia ndio ina mashirika ya kutoa misaada kwakuwa wenye haki hawakuwa na nguvu ya kutoa  ambapo sasa kuanzia leo mwovu hata jifiha kwenye Sadaka maana zote zimerejea kwa mpaji.

Yaani nguvu ya kutoa imerejea kwa MUNGU ambaye amempa Kanisa sasa.

Kurejea nguvu ya kutoa, maana kutoa ni:-
#Uhai
#Maisha
#Uzima
#Mafanikio
#Maongezeko
#Baraka
Nk. Vimehamia Madhabahuni.

Amesema vituo vote kanisa tumepita vikaibiwa leo kwa sadaka hii vitakuwa ni siraha ya kupiga waovu.

Yaani tuna hatua halisi ambayo ndio shamba. Leo wewe mwenye haki uliyeungana na MUNGU, Kristo na Kanisa unaAmri 1, hatma 1 halisi unatakiwa uwe na hakika zaidi.

Aidha Wakili wa MUNGU leo ametangaza mwisho wa mnyama asiyejulikana asiye na sura maalumu maana tuna uhalisi wa Isaya 62:1-3 kiti cha MUNGU hakikaliki akiwasambaratisha waliokaa popote walipokusanyana kinyume na kanisa.

Tunaungana na Jeshi la MUNGU kuondoa uchafu wote Amri 1 ya MUNGU ipo kazini kuondoa waovu wote.

Mwa 2:19 hata kama alimtuma Adamu alite yale majina aliita nayakawa ni yale yale akiwa amesimama hapohapo.

Kut 3:10 majira ya 3 MUNGU hakuwa na mahali pa kukanyaga kwasababu kila mahali palikuwa na pameharibiwa na kerubi.

Aliacha kukanyaga juu ya nchi kwasababu hakuona mahali pa kukanyaga akaona amtume Musa Kut 3:4-6.

Musa wakati anatumwa na MUNGU vitu vyote vilikuwa kwa kerubi na kerubi alikuwa ameshaathiri akili ya Musa.

Kwenye majira ya 5 wakamfuta Baba wakamuinua Yesu.

Hapawezekani kuwana kizazi pasipo kuwa na Mpakwa Mafuta, kwahiyo hata Musa alikuwa ni Kristo, mpakwa mafuta kizazi cha 1, Eliya Mtishibi alikuwa mpakwa mafuta kizazi cha 2 vitu vyote viligeuka kuwa mali ya kerubi.

MUNGU anakupaka mafuta kwa njia ya Sauti, kila kazi iliyofanywa na waliotumwa ni MUNGU alifanya.
Roho ndiye alikuwa wa Kwanza kumthibiti kerubi.

Yoh 20:1-9 alisema “Bwana wangu” sasa tambua anayeongoza kizazi siku zote huwa sio mtu. Hata kama utaona anafanana na wewe, anavaa kama wewe.

Yoh 19:30 akizungumzia kilichonyakuliwa 12 adar, 3 ni Roho ya Baba.
Amesema dunia ikiwa imekaa kuangalia macho juu kumsubili kristo mawinguni MUNGU aliwapiga chenga kristo akazliwa Kilimanjaro na sauti aliipata Kigoma akapakwa mafuta huko kwa agizo la kujenga kanisa.

Sauti ile ya MUNGU alipoipokea Eliya hakuwa tena mchaga bali NENO Kristo. MUNGU alianza na sasa anamalizia yeye mwenyewe ndio maana ni mwanzo a mwisho na alfa na omega.

Aidha akizungumziz kuhusu Eliya Ad2 na Wakili wa MUNGU amesema Zekalia 4:1-7 kuwa walikuwepo kabla ya misingi ya dunia kuwepo, kulia mwingine kushoto.

Aliongeza kuwa Eliya ndio sababu alipopata Sauti yaani majira ilipofika alienda kigoma kumtafuta miaka1000.

Hatahivyo Wakili wa MUNGU ameshirikisha wenye haki karamu ya umoja wa Baba, kristo na kanisa na kusema hakuna somo zaidi ya kushiriki pamoja kwenye sahani 1 bakuli 1kushiriki kwa mikono na ameagiza wenye haki wote kufanya hivyo.

Ambapo Wakili wa MUNGU alianza kuishirikisha familia yake ya viungo, familia ya mjumbe iliyowakirishwa na Mwaminifu, familia ya Mtendaji wa Wakili na makuhani wa NJia waliokuwepo na ndipo Kanisa zima tulishirikishwa karamu hiyo.


MAJIRA NA NYAKATI ZA HATMA HALISI KANISA LA  KWELI

Kanisa la kweli ni kusanyiko la watendao kwa haki. Yale aliyoyakusudia MUNGU tukiwa kwenye kiganja chake kuonekana kutimia kwa uhalisi sasa.

Awali akijenga msingi wa Ibada hiyo Wakili wa MUNGU aluimuhamisha kituo cha majina kiongozi wa makuhani ambapo sasa anaitwa "NJIA ZA BWANA" badala ya Njia za Bwana Ad2 MUNGU wa Majeshi" pamoja kuhani wa Kituo cha Ad2 "Kuhani YEHOSHANI".

Kinachowakamatia wengi ni kujiuliza maswali maswali kuwa Yesu ni nani? Eliya kizazi cha nne ni Nani na Miaka 1000 ni nani?

Ni MUNGU kabla ya majira ya 3 alikuwa hatumi bali alifanya mwenyewe.

MUNGU ana Nafsi 3 kwahiyo ukisema Nafsi ya MUNGU una maana ifuatayo 1 Yoh 5:8.

i)BABA ambaye ana moyo.
                               Roho
                               Nafsi

ii)NENO ambaye ana moyo.
                                Roho.
                               Nafsi.

iii)Roho ambaye ana moyo.
                                 Roho.
                                 Nafsi.                              

Huyu Baba ni MUNGU
        NENO- Kristo Mafuta.
        Roho - Kanisa

Hivyo kwa maana nyinge ukisema nafsi ya MUNGU un maana ya MUNGU kristo na Kanisa. Kwahiyo Kristo ni MUNGU na Kanisa ni MUNGU ndio sababu sio dini wala dhehebu.

Tunaenda mpaka mahali ambapomchawi, mzimu, ubya, uchafu haukubaliki ndani ya Kanisa kwasababu Kanisa ni MUNGU.

MUNGU ni mmoja
Nafsi ya 1 BABA
Nafsi ya 2 Neno - Kristo.
Nafsi ya 3 Roho - Kanisa.

Baada ya anguko hapa kwenye mlima wa MUNGU ndipo alipokuja na majira mpya mwanzo 1:3 siku zake 7.

 Akatengeneza Bustani ya Edeni. Anaposema tuumbe mtu kwa mfano wetu alikuwa na nani? Mwa 1:26 maana Nafsi yake ya 3 ambayo ni Roho tunamuona akiwa ni Mwa 1:2 kumthibiti kerubi aliyekuwa amekwisha geuka na kuwa shetani.

Mwanzoni tumemuona kuwa Baba ana nafsi ya:-
Baba - Moyo, Roho, Nafsi.
Neno - moyo, Roho, Nafsi.
Roho - moyo, roho, nafsi.

Katika Mwa1:26 alikuwa ni Roho wa Roho anaposema na tumuumbe. Baba wakati anamfukuza Ad1 pale bustani ya Edeni  katk Mwa 3:22-24.

Nguvu ya Moyo wa Roho. Roho na Nafsi ni moja. Wanaogopa Kanisa kwakuwa ni MUNGU hiyo ndio hatma halisi ya Neno.

Waliotumwa wote walikuwa ni wana. Kristo kizazi cha nne alikuwa na Roho ya Baba.

Mwa 18:3-10 Bwana akionekana kama watu watatu, ndio sababu nakuambia MUNGU anakula chips na mishikaki. Je pale kwa ibrahimu hakula?

Kumbe unaposema umezaliwa na mtu ni kosa, unaposema umefunuliwa Kanisa ni kosa kumbe MUNGU mwenyewe ndiye anayefunua Kanisa.

Baada ya kuiba nafsi hai ya Ad1 kerubi alienda kutengeneza majini. Mapepo, uchawi nk. Ndio maana Yesu ktk Mt 16:16 Nitalijenga Kanisa alikuwa na maana ya Roho.

Mt 3:15-17, 1 Petro 3:18 Roho wa kwa Neno.

Mdo 9:1-10, luka 24:50-51 aliyenyakuliwa ni Roho. Hivyo hivyo alivyoenda ndivyo atakavyorudi.

Yoh 17:4 Baba nimefanya kazi yako nirudishe kwenye utukufu wako wa kwanza kuwa NENO.

Yoh 9:7, Mt 21:40 Roho wa MUNGU ndio iliingia ndai ya Eliya akabadilika jina mpaka akakana malango ya mwanamke na mwanaume.

Aliyetufundisha kuhusu:-
*Vizazi vyote vine.
*Aliyevunja misingi mibaya.
*Aliyetuingiza kwenye majira mpya.
*Aliyesababisha tuvae vazi.
*Aliyekuja kujenga jukwaa la MUNGU kuja.
Alikuwa ni Roho wa BABA.

Kristo aliposema "Narudi kukaa kochi 1 na Baba ni Roho wa BABA. Huyo Roho alikuja na:-
#Matengenezo.
#Marejesho.
#Upatanisho.
#kujenga.
Huyo Baba ndiye mwenye hii Roho.

Kwahiyo hata huyo Roho wa Baba aliacha wenye hila na mashetani. Roho wa Baba ndiye alimwabia Miaka 1000 nimekuachia "wenye hila na mashetani usiwaogope waangamize waue wote"

Roho wa Baba hawezi kushindana na MUNGU ndio sababu Sasa tunaomba kwa Damu ya MUNGU.

Kanisa, Kristo na MUNGU ni kitu kimoja. Mimi ni Roho, Nafsi ya tatu ya MUNGU, nina Roho, moyo na Nafsi ya MUNGU.

Wakili wa MUNGU amesema kinachosumbua wengi ni kituo cha umbo la 1.

Aidha amewaonya makuhani kwa vituoni kumfafanua Wakili kama Aliyetumwa wakati yeye ni Aliyetuma kwasababu amembeba Aliyetuma ambaye anaishi kwake.

Kinachosumbua kingine kwenye maono ukimwona Wakili unasema leo nilimuona Miaka1000 kumbe ni MUNGU na Kristo. Amesema makuhani wengi wanapokwamia ni pale wanaposimama madhabahuni peke yao bila Wakili wa MUNGU wanajikuta wanafundisha vitu ambavyo ni vya level ya aliyetumwa ambavyo havimuamishi yeyote kituo.

"MUNGU hatambui kama niliwahi kuwepo majira ya 1-6, sauti ya 1-6 maana anajua hizo majira zote hazikuwahi kukupa haki ya kuishi, MUNGU anatambua kwamba majira hii ya 7 wenye haki ndio unaishi maana majira hii ndio inakupa haki ya kuishi.

Toba
Kutubu kwa MUNGU kwa roho tuliyokuwa nayo ya kulinganisha vitu na watu mwana nk.

OVYO
8 siwani,6 MUNGU amekuja kukaa nasi moja kwa moja. Tuwe tunaamkia madhabahuni. Sasa hivi MUNGU atakuwa anaua waovu wote.

Aidha Wakili wa MUNGU alihoji mwenye haki "kwani manataka kuishi au kufa?"

Hatahivyo Wakili wa MUNGU aliliongoza Kanisa kutoa Sadaka maalumu ya majira na nyakati za Hatma Halisi Kanisa la Kweli.

Ambapo pia Kiongozi wa Makuhani aliliongoza Kanisa toba ya kina ambayo ilihitimishwa kwa kutoa sadaka ya amani kati ya MUNGU na Kanisa.