Showing posts with label 20 Tamuzi 6. Show all posts
Showing posts with label 20 Tamuzi 6. Show all posts

Tuesday, 17 January 2017


PASAKA YA MUNGU KUGHAIRI MWANZO WA UHARIBIFU NA KUSIMAMISHA MWANZO MALIDADI MILELE

Wakili Wa MUNGU alianza kwa Shukrani kwa MUNGU na kusema Kama umeingia hapa una-huzuni, una-wazia unamdai/anaekudai, aliyekudhurumu una-mioyo sio MOYO.
MUNGU anaangalia Moyo sio Mioyo na Moyo huo uulinde
Hakikisha una-Moyo wa MUNGU, Moyo wa ni kumwabudu MUNGU katika Roho na Kweli.
Isa 14:13 Moyo wa MUNGU mahali pa Mlima wa Mkutano moyo wa kerubi mahali pa mlima wa Mungu.
Unapo-waza kinyume ina-maana una-moyo wa kerubi na moyo huo unatupwa chini.
Huyu anae-zuia usiwe na Moyo wa MUNGU leo tuna-shungulika nae.
Unapoambiwa Siloamu ni Mbaya wakati umepona na ukakubali huo ni moyo wa pili. Katika mda mfup unafurahi Neno ukitoka linayeyuka yaani una-ghairi Neno huo ni moyo wa pili.
Hiyo roho inayosababisha ughairi: Neno, utakatifu, kutenda mema.
#MUNGU Leo anaghairi Mwanzo wa uharibifu.
# MUNGU anaghairi alivyolighairi kanisa.
# MUNGU anaghairi kumuumba kerubi.
# MUNGU anaghairi kumuweka alama kaini kusema alindwe.
#Mungu anaghairi kuhusu mwenye HAKI kupigwa. Ayubu22:21.
MUNGU anaghairi kutokea kwa *mwanamke.
*nyoka
*anguko
*mioyo miwili.
Aidha Wakili aliongoza wenye HAKI kutoa Sadaka maalumu ya leo ni Kukaa na MOYO wa MUNGU wa kutenda mema Peke yake na mioyo mingine yote kufutwa kabisa.
Kuna namna ambayo unapata Hakika ya Neno halafu ghafla ukimwombea mwingine unasema; isipotokea je?
Hicho ndicho kinaiba Kile kilicho kuwa kimemeza uhalisi  wa kila ulichopewa na MUNGU kinamezwa badala ya kukumeza.
Ile doubt inayokuja baada ya kusikia NENO kinaungulia hapa kwenye sadaka.
Kile kitendo kutoka kanisani kwenda kwa mganga leo ni mwisho. Kila kinachotoka madhabahuni lazima kitimie.
Kutoka 24:12-, kutoka 32:7-8
Kizazi cha kwanza, hata kama umekwenda juu kiasi gani ama una moyo wa MUNGU kiasi gani ilikuwa  lazima ushuke chini.
Leo ni mwisho  na yote yaliokuwa ya kisababisha kushuka moyo leo MUNGU Anaondoka.
Leo moyo unapokuwa juu tu, ukijua kuwa MUNGU Anakuwazia mema tu.
Yeyote akikuletea taarifa mbaya mwambie ina muhusu kerubi
Yeremia 1:4-11 MUNGU hukuweka juu sana lakini unaona uko chini. Leo MUNGU Anakupeleka juu, usishuke tena. Usianagalie hali ulionayo tena.
Uibiwe usiibiwe, ona mema tu.
Leo MUNGU Anapokupeleka juu ,utashuka tena?
MUNGU Anapoachilia Moyo wake Mwenyewe hatarajii kuona ukiangalia mazingira tena.
-yohana 21:3-10 MUNGU Yuko hapa Anakupa vitu vizuri alafu unamwacha, je utapata kitu?
Kunawalioko hapa ambao wakiona msukosuko wanasema ng’oja nikae kwanza  nyumbani hadi hali hii iishe.
*Mahali  penye msukosuko kuna MUNGU,  kusipokuwa na msukosuko ina maana unatenda anayotaka kerubi.*
Wewe unapewa  na MUNGU vitu vikubwa alafu unakutana na msukosuko, unadondosha  chini?
Kwa sababu yeyote nisikute
Nafsi yako imeinama. "upokee furaha ya milele na kicheko cha milele".
"Nikikuona umeinama nafsi sitakusalimia na hata ukinisalimia sitaitikia" alisema Wakili wa MUNGU.
*Leo ni Pasaka ya MUNGU anaghairi mwanzo wa uharibifu milele na kusimamamisha Mwanzo Malidadi.*

Monday, 16 January 2017


KUFUNULIWA KWA KANISA LENYE MOYO MMOJA TU WA MUNGU

Wakili wa MUNGU Alianza ibada kwa uongoza wenye haki kutoa SADAKA YA: Kufuta agano la kutanguliwa kwa wenye HAKI Kila wanapotaka kushinda.
Ni sadaka ya kuishi ADEN na EDEN bila kutoka *kufika nimefika na kutoka sitoki*
Ni kusimamisha ukamilifu wa ushindi.
Kuingia EDEN na kukaa hapo hapo, baada ya kuondoa umbo la nyoka. Sasa tumefika kwenye ukamilifu wa ushindi.
Kuondoa agano la kutanguliwa kwa mwenye haki kila anapotaka kushinda. Katika kila eneo natangaza  ukamilifu wa ushindi kwa kuondoa agano la kutanguliwa.
Kanisa sio kwamba lilikuwa halija shinda, ukamilifu wa ushindi ulikuwa bado. Kila utakacho tamka ni lazima kitokee.
Leo tumepata ukamilifu wa ushindi, kazi ndio imeanza kwa mwenye haki kujiwekea ulinzi waovu wasikuvulie uchafu wao tena bali waokoke.
Mwa3:1-6, 3:1-3, moyo unaomwelekea MUNGU kwa kuongea sawa na Alichosema.
Mwa 3:4-6, moyo unaomwelekea kerubi kwa sababu ya kuamini uongo.
Hii ni mioyo miwili ndani ya mtu mmoja au ndani ya mwenye haki mmoja. Kuna kipindi unaongea kama MUNGU Alichosema, na kuna kipindi unaongea kama ndugu n.k nakuamini hata kama ni uongo.
SWALI: Ni kitu gani kilitokea hadi kerubi/ nyoka akafanikiwa kumdanganya mke wa Adam?
Mwa3:4-6, aliamini kuwa MUNGU nimbaya hataki tufanane naye.
Mkakati Katika Mwa3:4-6  nyoka alifanikiwa kuonyesha kwa mke wa Adam yaani kanisa kuwa MUNGU hampendi Adam, ila yeye kwa kuwa amewaibia  siri ndio mzuri.
MUNGU kuonekana mbaya, kerubi kuonekana mzuri.
Yale ambayo MUNGU Alikusudia kumpa Adam na mkewe hakupewa tena; Hiyo ndio hasara kwa kanisa. Hata vile alivyopewa Adam vilienda kwa kerubi.
Ndio maana mwenye haki kila anapofanya kizuri anaonekana kuwa anajipendekeza. Kila anachofanya mwenye haki kuonekana ni kibaya na mwovu kizuri.
MUNGU leo Anang’oa  kabisa huo moyo mwingine maana MUNGU Anataka moyo usio na mawazo wala makunyanzi.
Sasa moyo wa pili haupo tena na hauna nafasi tena ndani yako, ndani yako kuna moyo mmoja tu.
Moyo unaotokana na mataifa ulioenda, jamii, n.k haupo tena.
Sasa maongezeko yatakuwa makubwa maana kila kinacho toka hapa kinazaa matunda. Tumerudi katikati ya bustani ya EDEN hatutoki tena.
Ni wakati wa uzalishaji wa kumaanisha maana tumeingia CENTRE. Kile ambacho MUNGU Atakiachilia kwetu kitakaa hakitaibiwa tena. Kuna tabia ya kujihukumu kwa mwenye haki sasa tuache.
Nataka sasa umwambie MUNGU nitukanwe/ nisitukanwe kwenye kiini sitoki.
Yeyote akija kukuambia kinyume, mwambie kamwambie kerubi. Mimi sitoki.
+ufunuo 12:1-3 imefutwa kwa uhalisi.
+mwa1:2 Giza ukiwa na utupu mwisho.
+mwa2:8 mti wa ujuzi wa mema na mabaya umefutwa.
#kanisa tunakabidhiwa Mwa2:15 bustani kuilima na kuitunza.
Sasa MUNGU Anatuunganisha Na jeshi la:-
*kuwa na hakika ya safari kutimia.
*kuwa na hakika ya NENO kubarikiwa.
*kuwa na hakika ya kuinuliwa.
*kusudi la MUNGU kutokuzuiliwa na yeyote milele.
*aliyonena MUNGU yote yanatimia.
Ezekiel 36:26 MUNGU ametupa
#moyo MPYA.
#Roho mpya.
#Nafsi mpya.
Wakili amesema SILOAMU ambayo MUNGU alimpa Eliya Ad2 ndio imeanza Jana baada ya kufuta mioyo na tukabaki na Moyo.
Karibu usikilize ibada ya Leo upokee Moyo mmoja tu wa MUNGU.........